Shirika la habari la Palestina WAFA limesema Rais Mahmoud Abbas amekubali kujiuzulu kwa waziri mkuu Rami Hamdallah, na kukubali serikali yake ya sasa ya maafikiano kuendelea kufanya kazi hadi serikali mpya itakapoanzishwa. Shirika hilo pia limeripoti kuwa rais Abbas ataanza mazungumzo kuhusu kuanzishwa kwa serikali mpya itakayowashirikisha watu wa Chama cha Ukombozi wa Wapalestina PLO.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |