Mahakama kuu ya Venezuela imemzuia kiongozi wa upinzani Juan Guaido aliyejitangaza kuwa rais wa muda, kuondoka nchi hiyo na kuzuia mali zake. Uamuzi huo umekuja saa chache baada ya mwanasheria mkuu Tarek William Saab, kutangaza kuwa ameiomba mahakama kuu kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya Guaido.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |