Rais Edgar Lungu wa Zambia amewataka watu kuwalipa vizuri wasanii wanapotumia kazi zao.
Akizungumza na viongozi wa Baraza la Wasanii la Zambia, ikulu hapo jana, rais Lungu amesema Sanaa sio tu sehemu ya burudani lakini pia ni njia ya maisha kwa wasanii, na imekuwa ni sekta kubwa kwenye baadhi ya nchi.
Rais huyo pia ameeleza kuridhishwa na kazi za wasanii kwa kuwa zinaongeza kipato na kutoa nafasi ya ajira, na kuongeza kuwa ajenda kuu ya serikali ni kuhakikisha ajira na kuongeza kipato kwa wananchi wake, na kwamba sekta yoyote inayochangia ajenda hiyo inatakiwa kuungwa mkono.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |