Bandari ya nchi kavu inatarajiwa kujengwa eneo la Malula wilayani Arumeru mkoani Arusha nchini Tanzania lengo likiwa ni kuhudumia wafanyabiashara wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini na nchi jirani. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko alitoa taarifa hiyo kwenye kikao cha wafanyabishara ambapo aliongeza kuwa bandari hiyo itaanza kujengwa mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |