Kamisheni ya uchumi ya Umoja wa mataifa kwa nchi za Afrika ECA imesisitiza ahadi yake ya kuendelea kutoa uungaji mkono wa kiufundi kwa nchi za Afrika kwenye mipango yao ya maendeleo, katika ufunguzi wa mkutano wa siku mbili wa kati ya serikali uliofanyika jana mjini Addis Ababa.
Wataalamu kutoka taasisi za mipango na takwimu za Cameroon, Benin, Misri, Kenya, Zambia na zile kutoka ECA na mashirika mingine ya kimataifa wamehudhuria mkutano huo.
Nchi hizo tatu ni watangulizi wa Mradi wa 10 wa Akaunti ya Maendeleo wa Umoja wa mataifa kuhusu kuimarisha uwezo wa serikali za nchi za Afrika kwa ajili ya kuoanisha uwajibikaji kwenye mipango ya maendeleo ya taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |