• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Watu zaidi ya 60 wauawa katika mashambulizi nchini Nigeria

    (GMT+08:00) 2019-01-31 10:05:07

    Watu zaidi ya 60 wameuawa katika mashambulizi yaliyotokea kaskazini mashariki mwa Nigeria na kusababisha maelfu ya watu kukimbia makazi yao.

    Msemaji wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema kati ya watu 60 hadi 100 wameuawa katika shambulizi la wiki iliyopita. Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia mambo ya kibinadamu OCHA imesema, watu elfu 30 wamekimbilia Cameroon kutoka wilaya ya Rann, kaskazini mashariki mwa Nigeria ambapo wengine maelfu wamekimbilia eneo la Ngala na Maiduguri.

    Bw. Dujarric pia amesema, mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yameanzisha taratibu za kukabiliana na hali ya dharura na kutathmini mahitaji ya eneo la Ngala.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako