Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen Bw. Martin Griffiths amepongeza muungano unaoongozwa na Saudi Arabia kwa kuwaachia huru waasi wa Houthi ambao wamekabidhiwa kwa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu ICRC, siku moja baada ya kuachiwa huru kwa askari wa Saudi Arabia aliyekuwa mgonjwa. Amesema hatua hiyo inasaidia kuhimiza utekelezaji wa haraka wa makubaliano ya kubadilishana wafungwa. Hata hivyo, duru za kijeshi zinasema wapiganaji wa kundi la Houthi wameshambulia kwa mizinga viwanda vinavyomilikiwa na jeshi la serikali mjini Hodeidah, nchini Yemen.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |