Mkutano na wanahabari kuhusu tamasha la mwaka mpya wa jadi wa kichina la CCTV umefanyika hapa Beijing, na kufahamisha vipindi mbalimbali vya tamasha hilo na ubunifu mpya wa teknolojia utakaotumika katika tamasha hilo.
likiwa tamasha la kwanza tangu Kituo Kikuu cha Redio na Televisheni cha China (CMG) kizinduliwe, tamasha hilo lenye kauli mbiu ya "Kujiendeleza katika zama mpya, na kusherehekea mwaka mpya wenye baraka" litakuwa na maonesho mazuri ya nyimbo, ngoma, opera za kichina, michezo mifupi ya kuigiza na vichekesho.
Mwaka huu tamasha hilo litaoneshwa kwa mara ya kwanza kupitia majukwaa mbalimbali, ikiwemo televisheni, radio, APP na mitandao ya kijamii, na teknolojia ya 5G pia itatumiwa kwa mara ya kwanza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |