Waziri wa mambo wa nje Bw. Wang Yi amesema katika mwaka mpya China itaendelea kutekeleza kikamilifu fikra za rais Xi Jinping kuhusu masuala ya diplomasia, na kuendelea kufungua ukurasa mpya wa diplomasia za nchi kubwa zenye umaalumu wa kichina.
Akihutubia tafrija ya mwaka mpya kwa mabalozi na wajumbe wa mashirika ya kimataifa nchini China jana hapa Beijing, Bw. Wang Yi amesema, kamwe China haifanyi umwamba, na wala haitafuti kujipanua. China inashikilia kujenga aina mpya ya mahusiano ya kimataifa yenye haki na usawa, kuheshimiana na kunufaishana, na China inatumai kuwa nchi nyingine pia zitachagua na kufuata njia ya kujiendeleza kwa amani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |