Aussems amesema, baridi ndilo jambo lililowapa changamoto lakini kwa siku watakazokuwepo, watazoea na kuwa fiti kwa mchezo huo. Simba inatarajia kupambana na wenyeji Al Ahly katika mchezo wa kundi D kesho Jumamosi, mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Borg El Arab jijini Alexandria Misri.
Wakati hayo yakiendelea, wekundu hao wa Mismbazi wameweka wazi kuwa dili la kumtoa mshambuliaji wake mahiri Ramadhani Kichuya kwa mkopo kwa klabu ya Pharco limekamilika. Kichuya amesaini mkataba wa miaka 4 na klabu hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |