Shirika la wafanyakazi la Umoja wa Mataifa limehimiza serikali, sekta binafsi na jumuiya ya wafanyakazi za nchi za Afrika ziweke mkakati wa pamoja, ili kuongeza ajira zenye heshima.
Mtaalamu wa ajira ya vijana katika Shirika la Kazi Duniani ILO Bi. Susana Puerto akihudhuria kongamano mjini Nairobi, amesema vijana wengi wa Afrika wanafanya kazi kwenye sekta zisizo rasmi. Tunahimiza pande zote husika ziweke mkakati wa pamoja ili kuhakikisha vijana wa Afrika wanaweza kupata kazi rasmi.
Ameongeza kuwa hivi sasa takriban asilimia 12 ya wafanyakazi kutoka nchi za Afrika kusini mwa Sahara wamepoteza ajira. Vijana wengi wanabidi kufanya kazi kwenye sekta zisizo rasmi, ambazo haziwezi kuwapa ulinzi wa kijamii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |