• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Iran yapongeza Ulaya kudumisha biashara nayo ili kuepuka vikwazo vya Marekani

    (GMT+08:00) 2019-02-01 09:19:10

    Waziri wa mambo ya nje wa Iran Bw. Mohammad Javad Zarif amepongeza kuanzishwa kwa njia mpya ya malipo na nchi tatu za Ulaya Ufaransa, Ujerumani na Uingereza, ambazo zitasaidia makampuni ya nchi hizo kuendelea kufanya biashara na Iran.

    Bw. Zarif amesema, Iran iko tayari kuendelea kuwasiliana na nchi za Ulaya kwenye msingi wa kuheshimiana. Mapema siku hiyo Umoja wa Ulaya umetangaza kuanzisha shirika jipya la INSTEX kulinda biashara na Iran, ili kuepuka vikwazo vya Marekani, baada ya Marekani kujitoa kwenye makubaliano ya suala la nyuklia la Iran JCPOA.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako