Rais Donald Trump wa Marekani amesema tarehe na mahali pa kufanyika kwa mkutano wa pili kati yake na kiongozi mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, vimeamuliwa na vitatangazwa wiki ijayo. Pande hizo mbili zote zimeeleza kuwa na matarajio na mkutano huo. Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Jumatano alidokeza kuwa mkutano huo utafanyika barani Asia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |