Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema itaendelea kuchukua hatua kwa watoa huduma na watumiaji wa huduma za ubadilishaji fedha zisizo rasmi kwa sababu ni kinyume na sheria.
Hatua hiyo imefikiwa ikiwa ni siku chache tangu kufanyika kwa operesheni maalumu ya maduka ya kubadilisha fedha za kigeni Novemba 2018 jijini Arusha na kufungia baadhi ya maduka bubu ambayo hayana leseni yaliyokuwa yanaeendesha huduma hiyo kinyume na sheria.
Bot imezitaka taasisi za fedha kuendelea kutoa huduma ya ubadilishanaji fedha kwa watu wote wakati huu ambapo uchunguzi wa maduka bubu yaliyofungwa Arusha ukiendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |