Mpango huo unakuja wakati Tanzania ikipoteza hadi hekta 400,000 za miti kwa mwaka kutoka na uchomaji wa mkaa, kuni na matumizi mengine.
Kwa mujibu wa ripoti ya Mkakati wa Kitaifa wa Kudhibiti Misitu (Naforma) ya mwaka 2015, Tanzania ina eneo la hekta 48.2 milioni za misitu ikiwa ni sawa na asilimia 54.6 ya ardhi yote.
Ripoti hiyo inaonyesha kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye utajiri wa misitu ikiwa na mita za ujazo 3.3 bilioni za miti ya asili ambayo ni asilimia 97 ukiondoa miti ya kupandwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |