• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Serikali ya Tanzania yapanga kusambaza gesi ili kupunguza utumiaji wa makaa

    (GMT+08:00) 2019-02-05 18:38:15
    Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), linajipanga kutekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia kwenye makazi ya watu utakaofuta matumizi ya mkaa kwa ajili ya kupikia.

    Mpango huo unakuja wakati Tanzania ikipoteza hadi hekta 400,000 za miti kwa mwaka kutoka na uchomaji wa mkaa, kuni na matumizi mengine.

    Kwa mujibu wa ripoti ya Mkakati wa Kitaifa wa Kudhibiti Misitu (Naforma) ya mwaka 2015, Tanzania ina eneo la hekta 48.2 milioni za misitu ikiwa ni sawa na asilimia 54.6 ya ardhi yote.

    Ripoti hiyo inaonyesha kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye utajiri wa misitu ikiwa na mita za ujazo 3.3 bilioni za miti ya asili ambayo ni asilimia 97 ukiondoa miti ya kupandwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako