Wajumbe wa pande zenye mgogoro nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR wamesaini makubaliano ya amani huko Khartoum, mji mkuu wa Sudan, ambapo rais wa Sudan Omar al-Bashir na mwenzake wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Faustin-Archange Touadera wamehudhuria hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat amepongeza kusainiwa kwa makubaliano hayo, hatua ambayo amesema ni muhimu sana, na ameongeza kuwa changamoto ya sasa ni kama pande zenye mgogoro zitaweza kutekeleza kwa dhati vipengele vyote vilivyomo katika makubaliano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |