• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Serikali ya CAR na makundi 14 yasaini rasmi makubaliano ya amani

    (GMT+08:00) 2019-02-07 18:29:49

    Serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR na makundi 14 yenye silaha jana zimesaini rasmi makubaliano ya amani huko Bangui, mji mkuu wa nchi hiyo.

    Rais Faustin-Archange Touadera wa CAR amesema, serikali yake itajitahidi kutekeleza makubaliano hayo, na aina yoyote ya vitendo vya kimabavu dhidi ya raia yatatokomezwa.

    Mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika Bw. Moussa Faki aliyehudhuria shughuli ya kusaini makubaliano hayo, amesema changamoto halisi zitatokea baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo, Umoja wa Afrika utafuatilia kwa karibu utekelezaji wa makubaliano.

    Kwa sasa mambo halisi ya makubaliano hayajadokezwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako