Mwenyekiti wa mradi wa LAPSSET,Ttitus Ibui ambaye alikuwa ameandamana na maafisa wengine katia ziara ya bandari ya Lamu nchini Kenya alisema mradi huo wa ujenzi wa bandari ya Lamu utakamilika kwa wakati.
Alisema ujenzi wa eneo la kwanza la kuegesha meli katika bandari ya Lamu utakamilika mwisho wa mwezi Juni.
Serikali inatarajiwa kujenga maeneo matatu ya kwanza kuegesha meli kati ya 32 yatakayojengwa kwa gharama ya Sh48 bilioni.
Maeneo mengine mawili ya kuegesha meli yanatarajiwa kukamilika kufikia mwisho wa mwaka 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |