Ushindi katika vita huchagizwa na mambo mengi, licha ya kuwa na silaha bora, wingi na uimara wa kikosi cha wapiganaji dhidi ya wapinzani, bado mnaweza kupigwa na watu wanyonge wenye mbinu na mipango mujarabu. Ndivyo ilivyo katika soka, kesho jijini Dar es Salaam Tanzania wawakilishi wa Tanzania kwenye michuani ya klabu bingwa Afrika, Simba Sports Club watakuwa na kibarua kigumu dhidi ya mabingwa wa kihistoria wa Afrika, Al Ahly ya Misri.
Mtanange huu unakuja siku chache baada ya wekundu hao wa Msimbazi kukubali kipigo cha goli 5-0 nchini Misri, na sasa wanazisaka alama 3 kwa udi na uvumba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |