Kamishna wa Amani na Usalama wa Umoja wa Afrika Smail Chergui ametoa wito kwa nchi za kigeni kuacha kuingilia kati masuala ya Libya, nchi inayokabiliwa na vita. Akizungumza na waandishi wa habari kando ya mkutano wa 32 wa viongozi wa Umoja wa Afrika uliomalizika Addis Ababa, Ethiopia, Chergui amesema watu wa Libya wameteswa kutokana na vita vya ndani na nchi za kigeni kuingilia kati masuala ya nchi yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |