Wakulima wa chai nchini Kenya walipata shilingi bilioni 140 kutoka kwa mauzo ya bidhaa hiyo.
Mamlaka ya Usimamizi wa Chai imesema licha ya kuwa kulikuwa na uzalishaji wa juu bei ya kimataifa haikuathiri mapato.
Hayo ndio mapato ya juu zaidi kuwahi kupatikana ndani ya miaka 5 na ni ongezeko la shilingi bilioni 11 kutoka kwa mwaka 2017.
Uzalishaji ulifikia kilo milioni 474 ikilinganishwa na kilo milioni 415 za mwaka 2017.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |