Jeshi la anga la Nigeria limeanza kusambaza vifaa vya uchaguzi utakaofanyika Jumamosi. Msemaji wa jeshi hilo Ibikule Daramola amesema shughuli hizo zinafanyika saa 24 kila siku kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Azikwe mjini Abuja hadi viwanja vingine vya ndege nchini humo. Nigeria itafanya uchaguzi wa rais na wabunge siku ya Jumamosi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |