Ujerumani inahitaji wahamiaji wapya zaidi ya laki 2.6 kila mwaka hadi mwaka 2060 ili kutatua tatizo la upungufu wa nguvukazi linalosababishwa na kupungua kwa idadi ya watu. Kwa mujibu wa ripoti ya utafiti iliyotolewa na Mfuko wa Bertelsmann, kati ya wahamiaji hao wanaohitajika, watu wapatao laki 1.46 watahama kutoka nchi zisizo za Umoja wa Ulaya. Kazi za kiufundi zinahitaji wafanyakazi wengi kutoka nje.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |