Rais Omar al-Bashir wa Sudan amesema mwaka huu utakuwa mwaka wa amani kwa Sudan.
Akihutubia sherehe ya vikosi vya wanamgambo PDF mjini Khartoum, rais al-Bashir amesema mwaka huu utakuwa mwaka wa amani utakaotokomeza kabisa mapambano ya kisilaha nchini humo.
Rais al-Bashir amesisitiza ufuatiliaji wa serikali yake kwa vijana na kuwataja kama nguvu chanya, na kusema serikali yake inawajali vijana na inafanya juhudi kutimiza matarajio yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |