Mjumbe wa kudumu wa China kwenye Umoja wa mataifa balozi Ma Zhaoxu, jana alihutubia Umoja wa mataifa akieleza umuhimu wa suluhisho la kisiasa katika mgogoro wa Iraq.
Balozi Ma amesema kufikiwa kwa masikilizano shirikishi na kuwepo kwa pamoja katika hali ya masikilizano kwa vyama mbalimbali vya Iraq, kunaendana na maslahi ya kimsingi na mahitaji ya maendeleo ya watu wa Iraq.
Wito kama huo pia umetolewa na mjumbe mpya wa Umoja wa mataifa anayeshughulikia suala la Iraq Bibi Jeanine Hennis Plasschaert, ambaye amesema moyo wa ushirikiano kati ya makundi ya bunge, ulisaidia kuchaguliwa kwa waziri mkuu mpya miezi minne iliyopita. Hata hivyo tofauti kati ya pande hizo zimefanya nafasi nne muhimu za uwaziri kuendelea kuwa wazi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |