Mamlaka ya Mapato ya Uganda URA imeomba ile ya ushuru ya Kenya kuruhusu wataalam wa kuagiza na kusafirisha bidhaa wa Uganda kupata kwa rahisi huduma kwenye mifumo ya Kenya kama inavyofanyika Uganda.
Akizungumza kwenye hafla ya kuhitimu kwa Mazoezi ya Forodha Afrika Mashariki, kamishna wa URA Bw Dicksons Kateshumbwa, alisema kuwa zaidi ya wataalam 1,000 wa kusafirisha wa Kenya wanapata mifumo ya huduma kwa mizigo inayopelekwa Uganda.
Bwana Kateshumbwa amesema ataandika barua kwa Mamlaka ya Mapato ya Kenya ili kuomba kupewa idhini kwa mawakala wa kusafirisha wa Uganda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |