Serikali ya Rwanda imekanusha ripoti kwamba imepiga marufuku bidhaa kutoka Uganda ikitaja ripoti za vyombo vya habari kuwa potovu.
Maafisa wa wizara ya biashara nchini humo wamesema kuwa kupiga marufuku bidhaa za Uganga ni kinyume na makubaliano ya soko la pamoja ya soko huru la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Waziri wa maswala ya Afrika Mashariki wa Rwanda Olivier Nduhungirehe, amesema kuliwa na maswala kuhusu ubora wa bidhaa kutoka Uganda lakini yalishughulikiwa na halamashauri ya viwango nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |