Mchezaji mkongwe wa mchezo wa mieleka nchini Marekani, Ric Flair mwenye umri wa miaka 70 amenusurika kifo baada ya kuvamiwa na Batista kwenye vyumba vya kubadilishia nguo vya mchezo huo (WWE).
Tukio hilo limetoka jana ambapo mchezaji huyo mkongwe alikuwa akisheherekea kumbukumbu ya kuzaliwa. Triple H ndiye alikuwa mshehereshaji kwenye tukio hilo, baada ya kuona ukimya na kwenda nyuma ya jukwaa na kumkuta Flair amechakazwa vibaya na Batista, walimchukua na kumpatia huduma ya kwanza.
Tukio hilo linajiri katika kipindi ambacho Batista amepangiwa mchezo na Triple H, na inaelezwa kuwa amefanya hivyo kwa lengo la kumtisha
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |