SOKA: Matokeo ya michezo ya ligi Kuu Uingereza (EPL) iliyopigwa jana
(GMT+08:00) 2019-02-28 08:12:35
Ligi kuu ya Uingereza (EPL) imeendelea jana kwa michezo kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti, Arsenal imefanya maangamizi kwa kuipachika AFC Bournemouth mabao 5-1, Southampton wameibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Fulham, Nao watoto wa Stamford Bridge Chelsea wamepata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Tottenham Hotspur, Crystal Palace imejikuta ikikubali kipigo cha mabao 3-1 toka kwa Manchester United, Liverpool imeipa kichapo cha mwizi Watford cha magoli 5 nunge, na Manchester City imepata ushindi kiduchu wa goli 1-0 dhidi ya West Ham United.