Waziri mkuu wa China Li Keqiang leo kwenye ripoti ya kazi ya serikali amesema, mwaka huu idadi ya watu masikini vijijini nchini China itapungua kwa zaidi ya milioni 10.
Hatua za kupunguza umaskini zitakazochukuliwa mwaka huu ni pamoja na kuongeza nguvu za kuondoa umaskini kwenye maeneo maskini, kuunga mkono maendeleo ya sekta bora ya maeneo masikini, kupunguza idadi ya watoto wasiopata elimu kwenye maeneo hayo, na kuongeza idadi ya wanafunzi wa maeneo maskini wanaoandikishwa na vyuo vikuu muhimu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |