• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Wakulima kupata bima Tanzania

    (GMT+08:00) 2019-03-07 20:11:23
    Serikali ya Tanzania ipo kwenye mchakato wa kuanzisha bima ya mazao kwa wakulima ambayo itamsaidia kupata fidia pindi atakapopata majanga ikiwa mazao yake yataharibika kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

    Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Kilimo na Ushirika, Japhet Hasunga, wakati wa uzinduzi wa ushirikiano kati ya Mradi wa USAID -NAFAKA, na kampuni ya kimataifa ya Marekani ya uzalishaji na usambazaji mbegu na viuatilifu (Corteva).

    Waziri Hasunga alisema wakulima wamekuwa wakipata hasara baada ya mazao yao kuharibiwa na mafuriko, ukame pamoja na viwavijeshi licha ya kutumia gharama kubwa ya uzalishaji.

    Alisema serikali imeona changamoto hiyo na kwamba iko kwenye mkakati wa kuanzisha bima ya mazao kwa wakulima ambayo itakuwa mkombozi wakati wa majanga hayo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako