Ofisa Madini Mkazi wa Simanjiro, Daudi Ntalima, aliyasema hayo wakati akizungumza na wachimbaji wa madini ya tanzanite mji mdogo wa Mirerani.
Alisema mikataba yote wanayoingia na wageni inapaswa kusajiliwa wizarani na maelezo yatatolewa ofisini kwao.
Aliongeza kuwa wamiliki wa migodi wanapaswa kupewa utaratibu wa kusajili mikataba hiyo na serikali ikague kubaini namna watakavyonufaika na uwekezaji huo wa wageni.
Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Mkoa wa Manyara (Marema), Justine Nyari, alisema suala hilo watalifikisha kwa wachimbaji wote ili kuhakikisha mikataba yote ya uwekezaji inajulikana na kufikishwa ofisi ya madini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |