Shirika la ushirikiano na maendeleo ya uchumi hivi karibuni huko Paris limetoa ripoti ya mustakabali wa uchumi wa dunia na kupunguza makadirio ya ongezeko la uchumi wa dunia kwaa mwaka huu na mwaka kesho.
Ripoti hiyo imesema, uchumi wa dunia huenda utashuka kutokana na hali ya wasiwasi wa kibiashara, kupungua kwa uchumi wa Ulaya, udhaifu wa soko la fedha na kuporomoka kwa imani kwa biashara na matumizi. Ripoti hiyo imekadiria kuwa uchumi wa dunia utaongezeka kwa asilimia 3.3 katika mwaka huu na asilimia 3.4 mwaka kesho, makadirio hayo yamepungua kwa asilimia 0.2 na asilimia 0.1 kuliko makadirio yaliyotolewa mwezi Novemba mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |