Rais Xi Jinping wa China leo amesema China inapaswa kuhamasisha uwekezaji binafsi kuingia kwenye ujenzi wa miundombinu vijijini, ikiwa ni pamoja na uchukuzi, umwagiliaji, maji safi ya kunywa, na mtandao wa Internet, ili kutimiza lengo la kustawisha vijiji.
Kwenye mkutano wa mwaka huu wa Bunge la Umma, serikali ya China imesema itahakikisha malengo ya kupunguza umaskini na kuboresha maisha ya wakulima yanatimizwa kwa wakati.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |