Vyombo vya habari vya Israel vimesema hakuna majeruhi walioripotiwa kufuatia shambulizi hilo la roketi, baada ya kilichorushwa kuangukia kwenye eneo la wazi. Jeshi la Israeli limesema linachukulia jaribio lolote la kuwadhuru raia wa Israel kuwa ni kubwa, na itaendelea kwa dhamira kubwa kupambana na vitendo kama hivyo.
Kwa mujibu wa wizara ya afya ya Palestina, mwandamanaji Mpalestina aliuawa kwa risasi na wengine zaidi ya 40 kujeruhiwa katika mapambano na askari wa Israel yaliyotokea Ijumaa mpakani mwa Gaza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |