• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Kauli ya kwanza ya Zidane baada ya kutambulishwa Real Madrid

    (GMT+08:00) 2019-03-12 08:02:52

    Klabu ya Real Madrid jana imemtangaza rasmi kocha wao wa zamani Zinedine Zidane Zizzou kuwa ndio kocha wao mpya kwa mara ya nyingine tena ataitumikia klabu hiyo hadi mwaka 2022 hiyo ikiwa ni miezi 9 imepita toka kocha huyo alipoamua kujiuzulu baada ya ushindi wa tatu mfululizo wa ligi ya mabingwa Ulaya na ligi kuu ya Hispania.

    Klabu hiyo imeamua kumtupia virago aliyekuwa akiinoa timu hiyo Santiago Solari baada ya kushindwa kuleta mafanikio kwa klabu hiyo tangu alipotwaa mikoba.

    Akiongea na waandishi wa habari, Zidane amesema amerudi Madrid kwasababu rais amemuita na anafuraha kurudi na kuahidi timu inafanya vizuri kwakuwa watu wengi wanaipenda.

    Zidane alishahusishwa na mpango wa kujiunga na Chelsea kujaza nafasi ya Maurizio Sarru au Manchester United baada ya kumfukuza Jose Mourinho.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako