Wajasiriamali 30 kutoka Rwanda wamepata mafunzo ya biashara kutoka kwa chuo cha mafunzo ya biashara cha kampuni ya Alibaba mjini Hanghzou nchini China.
Mafunzo hayo yalihusu jinsi ya kupata uozefu wa kuendesha kwa ufanisi biashara ya mtandaoni.
Yametolewa chini ya ushirikiano wa Alibaba na halmashauri ya maendeleo ya Rwanda.
Mwaka jana Rwanda na alibaba zilisaini makubaliano ya kuwezesh bidhaa za Rwanda kama vile kahawa kuuzwa mtandaoni nchini China kupitia Alibaba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |