Makamu wa rais wa chama hicho, Paul Mutwii amewataja wanariadha hao ni Kibet Kandie na Agnes Mwikali waliokuwa katika vikosi vya wavulana na wasichana.
Kulingana na Mutwii, kuondolewa kwa wawili hao kulichangiwa na udanganyifu wa umri wakati wa mchujo wa kitaifa ulioandaliwa mjini Eldoret mwishoni mwa mwezi Februari.
Nafasi zao kwa sasa zimetwaliwa na Cleophas Kandie na Mercy Cherop. Hivi karibuni kuliibuka tetesi kwamba baadhi ya wanariadha waliowahi kuwakilisha taifa katika mashindano ya awali katika vitengo vya chipukizi walijitokeza kwa mara nyingine na vyeti ghushi vya kuzaliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |