Mwenyekiti wa kamati hiyo Hany Abo Rida ameiambia tovuti ya shirikisho la soka barani Africa (cafonline.com) kuwa, michuano hiyo itasalia katika kumbukumbu ya mashabiki wengi wa soka wakati na baada ya kumalizika.
Misri itakuwa nchi ya kwanza, kuandaa fainali hii ambayo kwa mara ya kwanza itakuwa na mataifa 24 katika michuano itakayoanza Juni 15 hadi Julai 13 mwaka huu.
Misri itatumia viwanja nane kwa mashindano hayo vilivyopo kwenye majiji matano tofauti: Alexandria, Ismailia, Port Said, Suez na mji mkuu wa Cairo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |