Wabunge wa Uingereza wamepiga kura na kuamua kuzuia nchi hiyo kujitoa Umoja wa Ulaya hadi makubaliano ya Brexit yatakapokubaliwa na umoja huo.
Mpango wa Brexit bila ya makubaliano umekataliwa na wabunge, na kutoa pigo kubwa kwa waziri mkuu wa nchi hiyo Bi. Theresa May. Kabla ya hapo, makubaliano yaliyorekebishwa ya Brexit pia yalikataliwa na wabunge.
Wabunge wa Uingereza wanatarajia kupiga kura za maoni tena kuhusu ombi la kuchelewesha muda wa mwisho wa Uingereza kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya ambalo ulikuwa tarehe 30, Juni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |