Uamuzi wa kuanza kutumia marefa wanawake katika mashindano ya wanaume ulifikiwa baada ya kamati ya marefa ya shirikisho la soka barani Afrika (CAF) katika kikao kilichofanyika Februari 26 mwaka huu makao makuu jijini Cairo nchini Misri na kuhudhuriwa na rais wa CAF, Ahmad Ahmad.
Marefa 15 na wasaidizi wao wa pembeni ambao ni washika vibendera 14 kutoka mataifa 25 wanachama, watafanyiwa ukaguzi wa kiafya, mazoezi ya uwanjani na pia kufanya mtihani ili kupata orodha ya mwisho ya maafisa wa kusimamia mechi wakati wa mashindano hayo yatakayoanza Aprili 14-28 mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |