• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Tiketi zaidi ya 100,000 zauzwa kuelekea kombe la dunia kwa vijana

    (GMT+08:00) 2019-03-15 07:49:48
    Shirikisho la soka duniani FIFA, limesema kuelekea fainali ya kombe la dunia kwa vijana wasiozidi miaka 20, tayari tiketi zaidi ya 100,000 zimeuzwa.

    Fainali hiyo itafanyika nchini Poland kati ya tarehe 23 mwezi Mei hadi Juni 15 mwaka 2019. Ripoti zinaonesha kuwa mashabiki wengi wamenunua tiketi za kushuhudia mechi ya ufunguzi kati ya wenyeji Poland na Colombia itakayochezwa katika uwanja wa Widzewa mjini Lodz.

    Wenyeji Poland wamepangwa katika kundi la A pamoja na Colombia, Tahiti na Senegal.

    Kundi B: Mexico, Italia, Japan na Ecuador.

    Kundi C: Honduras, New Zealand, Uruguay, Norway

    Kundi D: Qatar, Nigeria, Ukraine na Marekani

    Kundi E: Pana, Mali, Ufaransa, Saudi Arabia

    Kundi F: Ureno, Korea Kusini, Argentina, Afrika Kusini

    Mataifa 24 yatashiriki katika fainali hizo za 22 na bara la Afrika litawakilishwa na Senegal, Nigeria, Afrika Kusini na Mali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako