• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kamisheni ya UM yaitaka Israel irekebishe kanuni za uwepo wa kijeshi kabla ya maadhimisho ya Gaza

    (GMT+08:00) 2019-03-19 14:41:18

    Kamisheni Huru ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu maandamano katika Ukanda wa Gaza wa Palestina, imeitaka Israel kuhakikisha mara moja kuwa kanuni za uwepo wa vikosi vyake vya usalama zinarekebishwa, kwa kulingana na vigezo vya kisheria duniani. Kamisheni hiyo imewasilisha ripoti ya utafiti wake kwa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa baada ya kuchunguza mauaji yote na majeruhi yaliyosababishwa na vikosi hivyo katika eneo la kati ya Israel na Ukanda wa Gaza wakati wa maandamano ya mwaka jana. Ripoti imechunguza kwa makini amri za vikosi vya ulinzi vya Israel kutuma askari na kuchukua hatua zilizosababisha vifo vya waandamanaji wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako