Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deodatus Kakoko, alisema fedha hizo ni mpango wa kuchangia kupitia asilimia za mapato yake utakaotolewa katika maeneo muhimu ya kijamii kama elimu na afya.
Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi mabati 379 ya Shule ya Ufundi ya Tanga alisema pamoja na bati hizo, Mamlaka hiyo itachangia huduma za afya Wilaya ya Pangani.
Alisema uchangiaji huo ni utekelezaji wa sera ya Bodi ya Mamlaka hiyo na pia jamii inayoishi katika maeneo hususani yaliyozungukwa na Bandari na nchi nzima itanufaika na mpango huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |