Ikulu ya Marekani imetangaza kuwa rais Donald Trump amemteua Bw. Stephen Dickson, aliyekuwa rubani wa jeshi la anga na mkurugenzi wa shirika la ndege la Delta kuwa mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Marekani FAA. Uteuzi huo umekuja wakati ufuatiliaji unaongezeka kuhusu FAA kupitisha ndege za Boeing 737 Max. Taasisi ya uchunguzi wa usalama wa ndege ya nchini Ufaransa imesema, chanzo cha ajali ya ndege ya Boeing 737 Max 8 ya kampuni ya ndege ya Ethiopia kinafanana na kile cha ajali ya ndege ya Lion ya Indonesia iliyotokea mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |