Mwanariadha wa kike wa Kenya Joyciline Jepkosgei amenyakua taji la mbio fupi za jijini New York City nchini Marekani zilizofanyika mwishoni mwa wikiendi iliyopita.
Jepkosgei ameshinda taji jijini humo ambako Kenya haikuwa imetwaa taji la kinadada kwa miaka minne mfululizo. Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye anapanga kuanza kushindana katika mbio za kilomita 42 baadaye mwezi ujao, alikata utepe jijini New York kwa kutumia saa 1:10:07.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |