Kampuni ya Boeing yarejea ahadi yake ya usalama wa ndege kufuatia ajali ya ndege ya Ethiopia
Katika barua ya wazi iliyotolewa mwanzoni mwa wiki hii kwa mashirika ya ndege, abiria na jamii ya safari za anga, Bw. Muilenburg amezungumzia kuongezeka kwa wasiwasi kuhusu usalama wa ndege za kampuni hiyo kutokana na ajali mbaya ya ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia namba 302 iliyoanguka na kusababisha vifo vya abiria 157 pamoja na wahudumu.
Ajali hiyo ni ya pili inayohusisha ndege aina ya Boeing 737 MAX 8, baada ya ndege ya Indonesia Lion Air kuanguka mwezi Oktoba nchini Indonesia na kusababisha vifo vya watu 189.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |