Rais Xi Jinping wa China leo ameanza ziara yake rasmi nchini Italia, ambapo video ya "Hadithi zinazopendwa na Xi Jinping" ya lugha ya kiitalia ilivyotengenezwa na Shirika Kuu la Utangazaji la China CMG imeonyeshwa rasmi kwenye televisheni na tovuti za mashirika ya habari Mediaset na Class Editori nchini Italia.
Kabla ya hapo, video hiyo ilitafsiriwa kwa lugha za Kiingereza, Kijapan, Kikorea na Kihispania, na kuonyeshwa kwa zaidi ya watazamaji milioni 100 wa nchi za nje.
Video hiyo imekusanya methali na maneno maarufu ya hadithi za kichina ambazo zilitumiwa na rais Xi kwenye hotuba na makala zake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |