Mashindano ya dunia ya kuteleza kwenye sakafu ya barafu ya mwaka huu yameanza nchini Japan katika uwanja wa Saitama, jumla ya medali nne kushindaniwa katika vitengo vya wanaume, wanawake, jozi ya wawili na kucheza muziki.
Mabingwa wa ulaya wa mwaka huu wanaoshiriki katika kitengo cha jozi ya wawili, Vanessa James na Morgan Cipre kutoka Ufaransa wanakabiliwa na michezo mgumu watakaposhindana na jozi za washindi wa medali ya fedha wa Olimpiki toka China, Wengjing Sui na Cong Han, pia na jozi nyingine ya washindi wa medali ya fedha wa mwaka 2018 kutoka Russia, Evgenia Tarasova na Vladimir Morozov na kumaliza na jozi ya Zoe Jones anayeshirikiana na Christopher Boyadji wa Uingereza.
Mashindano hayo yatafikia tamati kesho kutwa Jumapili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |