Waziri wa Ofisi ya makamu wa rais anayeshughulikia mambo ya muungano na mazingira wa Tanzania Bw. Januari Makamba, amesema nchi hiyo imesimamisha uingizaji, usafirishaji nje ya nchi, uchakataji na ukusanyaji wa taka hatari hadi mfumo mpya wa kusimamia shughuli hizo za biashara utakapotangazwa.
Waziri huyo amesema kupitia taarifa kwamba taka hizo ni pamoja na vyuma chakavu, betri zilizotumika na taka za kielektroniki. Vilevile amepiga marufuku wafanyabiashara kupokea taka hatari kutoka kwa mtu yeyote asiye na idhini kutoka ofisi ya makamu wa rais
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |